Latest Posts

06 February, 2016

RISALA YA MWENYEKITI WA WAGANGA WA MARUHANIA.

·        Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa
·        Afisa Maendeleo wa Mtaa
·        Mwenyekiti wa Kamati ya Afya na Mazingira
·        Wajumbe wa Serikali ya Mtaa
·        Mwenyekiti wa Maruhania
·        Katibu wa Maruhania
·        Waganga Mafundi, Walimu wa Maruhania (Watabibu wa Tiba Asilia)
·        Mabibi na Mabwana.
Habari za Muda huu
Leo ni siku ya pekee kwa wanamaruhania na watu wote wanaopenda maendeleo yetu na hasa katika tiba asilia na afya ya watanzania. Ni siku ambayo tunaandika historia katika Tiba Asilia na Maruhania. Kihistoria hakuna anayefahamu kwa hakika lini ushirikiano kati ya mwanadamu na Maruhani katika kutoa huduma ya Tiba Asilia na ilianza lini kutumika hapa kwetu Tanzania ila kila mmoja wetu atakubariana kuwa ilianza tuu pale binadamu wa kwanza alipoanza kuishi katika nchi yetu kwa miaka yote ya kuwepo kwa binadamu hapa Tanzania, Tiba ya kiruhani nayo imekuwa muhimili wa matibabu ya Tiba Asili.
Pamoja na kuwepo kwa maendeleo makubwa katika teknolojia na usambazaji wa huduma ya Tiba ya kisasa nchini kote lakini tiba ya maruhani asilia bado inaendelea kutumiwa na wananchi wengi, wa mijini na vijijini. Pamoja na Tiba ya kiruhani kutumiwa na wananchi wengi, huduma hii imekuwa ikitolewa katika mgumo usio rasmi, hali hii imekuwa ikichangia na kuifanya Tiba ya maruhani, isikubaliwe na watu wengi wasomi na Imani za mapokeo yasiyo ya asili ya mwafrika na mtanzania.
Kwakuwa serikali inatambua umuhimu wa Tiba Asilia hivyo kuanzia mwaka 1961 imekuwa ikichukuwa hatua mbalimbali kwa nia ya kuboresha huduma hiyo kwa kuweka sera, sheria, kanuni, miongozo na mikakati mbalimbali ya uendelezaji na uimalishaji.
Hatua hizo ni pamoja na kuanzisha taasisi za utafiti katika Tiba Asili, kuimalisha huduma za Tiba Asili kwa kuanzishwa kwa kitengo cha Tiba Asili, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Kujuishwa kwa Tiba Asili katika Sera ya Taifa ya Afya yam waka 1990, kutungwa kwa Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala Namba 23 ya Mwaka 2002 na Kuanzishwa kwa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala kuanzia Mwaka 2005.
Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala kwa Kushirikiana na Kitengo cha Tiba Asili, Imejikita katika Kutunga kanuni na Kutengeneza miongozo Mbalimbali ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kuwasajili waganga na Wakunga wa Tiba Asili nchini ili kuimarisha utekelezaji wa Sheria namba 23 ya mwaka 2002, Sera, kanuni na Miongozo mbalimbali imekwisha sambazwa katika ofisi za waganga wakuu wa mikoa, wilaya,halmashauri za miji na Majiji na mpango wa maendeleo wa Afya ya Msingi wa mwaka  2007 – 2017.Vile vile Wizara imekuwa ikitoa elimu kuhusu Tiba Asili kupitia vyombo vya habari na maonesho ya kitaifa ya Tiba Asili na itaendelea kufanya hivyo.
Ndugu zangu wana Maruhani uhimalishaji wa Tiba Asili unajumuisha:-
·        Usajili wa Waganga, Wakunga na Wauza dawa wa Tiba Asili
·        Uanzishwaji na Usajili wa Vituo rasmi na Vilivyo bora vya kutolea huduma za Tiba Asili na Vinavyokidhi viwango vya Afya.
·        Utafiti na Utengenezaji wa Dawa unaokidhi viwango vya ubora, usalama na uwezo wa Kutibu.
·        Uanzishwaji wa kilimo cha miti dawa ili kuboresha dawa na mazingira.
·        Uwepo wa taratibu za usimamizi na udhibiti wa huduma ya Tiba Asili na Maruhania katika kutoa huduma ya Tiba Asili katika kila halmashauri ya Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji.
Kwahiyo nawaomba kila Mganga wa Maruhania afuate maelezo yaliyotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia Wazee na Watoto tarehe 15/ januari 2016, juu ya utolewaji wa huduma za Afya kwa Tiba Asili na Tiba Mbadala hapa nchini
hapa nchini kuna Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu za maadili zinazotutaka tuzitii bira shuruti. Ni muhimu kwa kila mtoa huduma ya Afya kwa Tiba Asili ya Maruhani kutoa huduma kwa kuzingatia miongozo ya utoaji wa huduma hizo.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Watu wake wanathamini Tiba Asili na Tiba Mbadala, kwani Tiba Asilia ni Mama wa Tiba ya Kisasa. Sayansi ya Tiba ya Kisasa inatambua sayansi ya Tiba Asilia.
Hata hivyo huduma ya Tiba Asilia na Tiba Mbadala inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na :-
·        kutotambuliwa na baadhi ya watoa huduma wa Tiba za Kisasa kwa sababu mitaala ya mafunzo ya wataalam wa Tiba za Kisasa(Madaktari, wafamasia na Manesi) imewanyima fursa ya kupata maarifa juu ya Tiba Asilia na matumizi yake katika tiba.
·        Katika Jamii pia kumekuwepo na Imani potofu kwa baadhi ya jamii wakihusisha Tiba Asilia na Imani za kishirikina.

·        Ukosekanaji wa fedha za Utafiti umesababisha kukosekana kwa utengenezaji wa dawa zinazokidhi viwango vya ubora, Usalama na Uwezo wa Kutibu na kuzisajiri dawa hizo kwenye mamlaka zinazohusika kwa mujibu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo iliyopo.
·        Uhifadhi mbaya wa mashamba ya Miti dawa ili mitidawa hiyo iweze kufanyiwa utafiti na kuwa dawa bora na salama pamoja na utunzaji endelevu wa mazingira
·        Pia kunachangamoto ya  Uendelezaji wa Wataalam wa Tiba Asili kitaaluma ili wawe na uwezo wa kuboresha huduma zao baada ya kusajiliwa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala Kukosekana kwa Muongozo wa ajira za utumishi katika sekta ya Tiba Asili.
Kama tulivyoahidi kuwa tutakuwa na mikutano ya uhamasishaji tunatowa shukurani kwa viongozi wa maruhani kuja kwenye mkutano huu na kujadiliana njia bora ya kufuata maelekezo ya Mhe. Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto juu ya utowaji wa huduma ya Afya kwa Tiba Asili na Tiba Mbadala.
Walimu waambieni Maruhani kuwa Kuna agizo la Serikali linalotakiwa lifuatwe na Viti wao ili viti wao wasije wakapatwa na matatizo ya kisheria yaliyopitishwa katika nchi yetu ya Tanzania katika kutowa huduma ya Tiba Asili pia wafikishieni ujumbe huu watu wote walio na maruhani ambao wanatoa huduma ya Tiba Asili kwa kupitia Maruhani.
Ndugu viongozi wa koo za kiganga na mafundi wake, TRAMEPRO inataka viongozi wa koo za waganga wajitayarishe, tutaendelea na mkutano ya pamoja ili tutambike, ili waganga waliopo katika mila na desturi za kiganga wachukue fomu, kila mila itambike ili waganga wachukuwe fomu na kuanza kufuata utaratibu wa kisheria.
Baadhi ya makundi ya koo za kiganga na watoto wa dawa popote walipo tunataka viongozi wao, Walua, Wabisa, Waswezi, Watongwe, Ruhania, Waganga wa vitabu, Kidama, Kimbunga, Shimbalyoto, Kikola, Ndandi, Matepula, Mbei, lyamite, Shuma, Makamanda, Chambuya, Mchela, Kinyamkela, Lungu Likoko na koo nyingine zote.
Waganga tutowe huduma zetu kwa mfumo wa taasisi na siyo mtu mmoja mmoja kama ilivyo sasa kwa kuanzisha vituo rasmi kwa Mujibu wa Sheria, kanuni na Miongozo, ili iwe rahisi kupata mafunzo yanayostahili kwa huduma tunazozitoa kwa jamii.
Tayarisheni dawa katika sehemu maalum zenye mazingira ya usafi na salama ili kuepuka matumizi ya dawa zinazoweza kuleta madhara pamoja kutunza kumbukumbu kwa kuandika taarifa za ugonjwa na wagonjwa.
Tunaandaa mafunzo ya kuendeleza elimu na taaluma ya Tiba Asili ili mganga awe na uwezo wa kuboresha huduma azitoazo.
Kwa hivi sasa kutakuwa na uratibu wa kila Ngariba wanaotahiri wanaume ili wapate mafunzo maalum ya huduma waitoayo kwa jamii katika kulinda Afya ya Ngaliba mwenyewe na Muhitaji.
Waganga wa Tiba Asili, wauza duka la dawa asili, Wakunga wa Tiba asili, Ngariba wa wanaume, wenye viwanda vidogo vidogo vya utengenezaji wa dawa na wasaidizi wao tujisajiri kwa kipindi hiki cha miezi mitatu (3) na Vijijini tuzingatie miezi sita(6) tuliyopewa ili kuepuka hatua kali za kisheria zitakazo chukuliwa kwa kupuuza kusajiliwa katika kipindi kilichowekwa.
Shirika lenu la dawa asilia na ulinzi wa mazingira (TRAMEPRO) kwa kushirikiana na Watoa huduma wa Tiba Asili kwa ngazi zote , wasimamizi katika ngazi za maamuzi na wadau wote wa Tiba Asili tushirikiane kuitikia wito wa Serikali ili tuweze kupata na kutoa huduma zilizo bora na Salama.
Kwa changamoto zozote zitakazojitokeza katika kipindi cha kutekeleza agizo la Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia Wazee na watoto kwa Tiba Asili na Tiba Mbadala, tuwasiliane ili kupata ufumbuzi wa pamoja kabla ya muda haujamalizika yaani kabla ya Tarehe 15/April, 2016 kwa mjini na tarehe 15/Julai, 2016 kwa vijijini.
Lengo ni Kuona jamii ya watanzania inafikia malengo yake bila kuwepo kwa magonjwa, maisha bora kwaujumla kupitia dawa asilia na mazingira salama na yaliyotunzwa yanayo wazunguka.


ATHUMANI S. UNGANDO
MWENYEKITI, WAMARUHANIA

04/02/ 2016

17 March, 2015

TIBA ASILI BADO IMEGUBIKWA NA CHANGAMOTO

 AGOSTI 31 mwaka huu kulikuwa na Maadhimisho ya Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika yaliyofanyika Zanzibar katika viwanja vya Bustani ya Victoria mjini humo.
Moja ya mambo yaliyosisitizwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein, kupitia hotuba yake iliyosomwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, ni pamoja na kukemea baadhi ya watu kisiwani humo wanaojitangaza kupitia baadhi ya misikiti na mabaraza kuwa wana uwezo wa kutoa Tiba Asili, akisema kufanya hivyo ni kinyume na sheria.



Lakini pia hakusita kusema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inalipa kipaumbele suala la utafiti wa Tiba Asili na kuwa kuna uhusiano mzuri kati ya Wizara ya Afya na chama cha Watabibu Asili visiwani humo. Mwisho akaagiza mamlaka husika kushughulikia tatizo hilo.

Caroline mtafiti  wa tiba Asili kutoka chuo kikuu cha Berlin Ujerumani akipata maelezo kutoka kwa Mtabibu na Mtafiti wa Tiba Asili Bwana Boniventura Mwalongo ambaye pia ni Katibu wa ASSOCIATION OF TRADITIONA AND ALTERNATIVE MEDICINE IN EAST AFRIKA kutoka Tanzania  
Awali akisoma hotuba yake katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala Zanzibar, Mayassa Salum Ally Alisema kuwa Wizara ya Afya kupitia baraza hilo imefanya jitihada mbali mbali kuinua Tiba Asili na Tiba Mbadala na kufanikiwa kuongeza idadi ya wataalamu hao ambapo sasa kuna watabibu 193 waliosajiliwa na kuna jumla ya kliniki 18 na vilinge  125.

 Rais wa chama cha Tiba Asili na Tiba Mbadala Afrika Mashariki Lyidia Matoke Akitoa Maelezo kuhusu Tiba Asili Kwa Makamu wa Kwanza wa Rais  wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad

Sera ya Taifa ya Afya inaonyesha kuwa kabla ya Uhuru, huduma za afya zilikuwa zikitolewa zaidi katika maeneo ya shughuli za kiuchumi kama miji na mashanba makubwa. Baada ya Uhuru serikali iliweka msukumo zaidi katika kupanua huduma za afya ili kuwafikia wananchi walio wengi, hasa walioko maeneo ya vijijini.
Tiba Asili na Tiba Mbadala imekuwa ikishika kasi kila kukicha, japokuwa kuna changamoto za hapa na pale. Kuna haja ya kukubali kuwa changamoto nyingi zinazotokea katika eneo hili la Tiba Asili na Tiba Mbadala huenda zinatokana na ukosefu wa elimu ya kutosha kwa watanzania walio wengi ambao mara nyingi wamekuwa wakishindwa kutofautisha Tiba Asili na tiba nyingine zinazotolewa kwa kisingizio cha mtindo huo.
Kutokana na mkanganyiko huu, kumekuwa na tafsri za aina tofauti juu ya aina za waganga. Katika imani za kawaida, kuna aina tatu za waganga: Waganga wa Asili, Waganga wa Jadi na Waganga wa Kienyeji.
Kutokana na tafsiri inayotolewa na Chama Cha Utabibu Asili Tanzania (ATME),  Mganga wa asili ni yule anaye shughulika na tiba za maradhi kwa kutumia dawa za asili, kutibu maradhi  kwa binadamu, wanyama mimea kwa kufuata maadili ya utoaji huduma ya matibabu
Mganga wa Jadi: Anatumia Mila na Desturi katika tiba na utoaji dawa kwa wagonjwa iwe binadamu, wanyama, mimea. Hutegemea zaidi mila na desturi pamoja na tiba asili na dawa za asili kama kanuni na maadili ya utoaji huduma ya tiba.

Mganga wa kienyeji: Hana mafunzo maalumu ya tiba ya upande wowote wa tiba katika utoaji wake wa huduma kwa jamii. Ni mtu anayeweza kuchanganya taaluma mbalimbali hata za kisayansi ili mradi afanikishe alichokusudia. Mganga huyo pia anaweza kutumia vazi lolote liwe la Sheikh, Askofu, Daktari, Mganga wa Asili, ilimradi afikie lengo lake.

ATME wanasisitiza kuwa, mganga yoyote mwenye fani nzuri akiitumia katika kutenda maovu, huyo ndiye mganga wa kienyeji na wala si mtaalamu wa Tiba za Asili.
Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), takribani 60% ya wananchi huanza kutumia tiba asilia wanapopatwa na maradhi kabla ya kwenda vituo vya kutolea huduma za afya.
Nchini Tanzania Tiba Asili imekuwa na changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni ile ya baadhi ya watu kuihusisha na vitendo vya kishirikina, hali ambayo ni kinyume na sheria na taratibu zake, lakini pia kupotosha jamii.
Kwa mujibu wa Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala ya mwaka 2002, watabibu wote wa Tiba Asilia na Mbadala wako chini ya Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala ambalo mbali na majukumu mengine lina jukumu la kusajili watabibu wote wenye sifa zinazotakiwa baada ya kuwafanyia usaili. Lakini pia kuendeleza na kuboresha huduma hiyo.
Moja ya mikakati ya Baraza hilo kwasasa ni kuhakikisha kuhakikisha kuwa watabibu wote wa Tiba Asili wanapata usajili, ili kudhibiti vitendo vinavyotishia maisha ya binadamu ambavyo vimekuwa vikihusishwa na Tiba Asili.
Baraza linakiri kuwa ni kweli kuwa kuna idadi kubwa ya watu anbao wanajihusisha na huduma ya tiba asili kinyemela, kitu ambacho ni kinyume na sheria. 
Katika semina ya vyombo vya habari iliyoandaliwa na ATME jijini Dar es Salaam Mei 15 mwaka huu katika Ukumbi wa NMR Dar es Salaam,  Mlezi wa chama hicho, Kingunge Ngombale Mwiru alisema Watanzania wengi ni wazito  kukubaliana na Tiba Asili, hali ambayo alisema inachangiwa na dhana ya kutawaliwa na wakoloni.
Mwenyekiti wa ATME Simba Abdulhamani Simba anasema kuna umuhimu wa serikali kuhakikisha kuwa watabibu wote wa tiba asili wanasajiliwa ili kupunguza matukio ambayo yamekuwa yakifanywa na baadhi ya watu wanaojiita wataalamu  wa tiba, lakini kwa kuichanganya na vitendo vya kishirikina.
Boninventure Mwalongo ni Mkurugenzi wa Kliniki ya Tiba Asili ya Boresa ya jijini Dar es Salaam ambaye pia ni Mratibu wa ATME, anasema kuwa kwa sasa wako katika mkakati wa kuhakikisha wanawashirikisha wadau mbalimbali ili jamii itambue umuhimu

wa tiba asili, ikiwa ni pamoja na kutoa semina kwa wadau mbalimbali.

Mwalongo anasema kuwa jambo jingine ambalo linatakiwa kudhibitiwa ni matangazo holela ya waganga ambayo yamekuwa yakibadikwa na hata mengine kutumika katika vyombo vya habari bila kufuata utaratibu.
Aidha kumekuwa na uhusiano wa karibu kati ya wadau wa Tiba Asili na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA). Mwaka 2012 kulikuwa na mkutano wa wadau wa dawa za asili. Halikadhalika Novemba 5 mwaka jana TFDA walikutana tena na wadau wa Tiba Asili.
Moja ya malengo ya mkutano huo ilikuwa ni pamoja na kukumbushana matakwa ya sheria pamoja na changamoto za udhibiti. Katika Mkutano huoMkurugenzi Mkuu waTFDA, Hiiti Sillo alisema kuwa moja ya changamoto katika Tiba Asili na Tiba Mbadala ni kuwepo katika soko bila kufuata taratibu za utengenezaji, lakini pia akasema akaongelea juu ya baadhi ya watu kutoa matangazo katika vyombo vya habari pasipo vibali vya Mamlaka hiyo.
Mwalongo anasema kuwa mikutano kama hiyo inadhihirisha jinsi Tiba Asili inavyozidi kupata uigo na kuzidi kuthaminiwa na kwamba watanzania wanapata mwanga zaidi wa kutambua kilicho bora na kuepuka udanganyifu kwa baadhi ya watu wanaojiita watabibu asili kinyume na utaratibu.
“Kwa ushirikiano kama huu nafikiri tutafika mahala watanzania walio wengi watafahamu umuhimu wa Tiba Asili kama ilivyo katika nchi za India na China ambako kwa mujibu wa takwimu za nchi hizo asilimia 80 za raia katika nchi hizo wanategemea Tiba Asili.
Ends.

WATAALAMU WA TIBA ASILI WAKUTANA CHINI YA JUKWAA MOJA; WAONYESHA UMAHIRI KATIKA TIBA ASILI NA MBADALA

Mratibu wa Jukwaa la Tiba Asili Tanzania, Boniventura F. Mwalongo akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja yalikofanyika Maonyesho ya Tiba Asili na Mbadala


Dr. Jumanne wa Huduma ya Uponyaji akimsikiliza mmoja wa waliotembelea Banda lake kwenye Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Tiba  zinazotolewa na Dk. Jumanne ni zile zinazotokana na Matunda na Mboga Mbalmbali . Simu 0755087303





Dk. Salimu akiwaeleza watu waliofika kwenye maonyesho ya dawa asili jinsi dawa zake zinavyofanya kazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja


Dk.Ahmad Darusi Salimu Mkurugenzi wa M. M.D.K Clinic akitoa maelezo ya jinsi dawa zake zinavyotakiwa kutumika. Yeye amebobea katika kutibu Kansa za aina zote na pia anayo dawa inayosaidia kuondoa magonjwa nyemelezi kwa wagonjwa wa UKIMWI. Simu 0754467406, 0787467406

Mkurugenzi wa Kampuniya Dk.Fadhili Herbal Medicine & Nutritional,akitoa maelezo kwa wateja ((hawapo pichani) waliofika kwenye Banda lake wakati wa Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala yaliyofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja hivi Karibuni.  Dk. Fadhili pia ni Mshauri wa Afya katika Kampuni ya BF SUMA kutoka Marekani inayojishuhulisha na usambazaji wa dawa zenye Virutubisho vinavyoweza kuongeza kinga ya mwili (CD4) kwa 100%, kurekebisha Sukari na zingine nyingi.  Simu 0713834556

Dk. Nyakubaho (katikati) Mkurugenzi wa Kikundi cha tiba Asili cha Nyakiziba Shunga Tradtional Clinic. Wanazo dawa nyingi za kutibu maradhi mbalimbali kama inavyoonekana Pichani. Simu 0784936177, 0755570321

Bi EmilianaKokuhumuliza, Mtabibu wa asili anayetibu kwa kutumia mitishamba kutoka Mkoa wa Kagera. anapatikana Mjini Morogoro. Simu 0766903297. Picha zote na Muchunguzi Kamugisha wa ZUNGU

mhe.Kingunge Ngombale Mwilu akitembelea moja ya mabanda katika maonesho ya kwanza ya kimataifa ya tiba asili ya mwafrika
























































NAKUPENDA TANZANIA

Flag Counter

Popular Posts

Recent Posts

Flag Counter

Unordered List

Text Widget